Monday, March 29, 2010

THE KING IS BACK.

Clifford “T.I.” Harris yupo huru hivi sasa mara baada ya kutumikia kifungo cha mwaka m1 jela kwa kosa la kutumia silaha kinyume na sheria kwa mujibu wa mwanasheria wa TI Steve Sadow amesema kuwa licha ya jamaa kumaliza kifungo hicho lakini bado yupo katika muda wa probation kwa muda wa miaka mitatu, kwa muda huo atatakiwa kuwa anareport kwa maofisa wa police ambao amepangiwa na kutoa taarifa katika safari anazotaka kuziofanya na pia kufanya kazi za kijamii kwa muda usio pungua dakika 400
Lakini wakili wa mkali huyo amesema TI anaruhusiwa kuendelea kufanya kazi zake binafsi ikiwemo kurecord tracks na kufanya show tofauti tofauti.
jamaa anajipanga kutoka na albamu yake mpya August 24 mwaka huu na . B.o.B na Jim Jonsin ni moja kati ya maproduce watakao shioriki katika albamu hiyo
The King is back.

Thursday, March 25, 2010

HAPPY BIRTHDAY KIDUCHU!

Anaitwa argines samson anderson (kiduchu)leo ni siku yenye kumbukumbu kubwa kwake  dizain kama amezaliwa upya vile.....Anywayz twentyfoursevenmishemishe inakutakikia baraka tele...
(picha :hidhini ya http://www.kiduchu.blogspot.com/) ONE.

SNOOP"AMKUBALI JUSTIN BIEBER


Kupitia interview aliofanya snoop na MTV UK, rapper ameonesha kumkubali dogo anayekuja kwa kasi katika Justin Bieber
Snoop amesema alifanikiwa kukutana live na dogo huyo ameye amesema ni mpole ukimtizama na anatarajia atakuwa mkali zaidi siku za usoni kwa kuwa bado mdogo na anaamini kipaji chake kinakuwa pia
Bieber na Snoop Dogg kwa pamoja juzi March 23 waliachia kazi zao mpya Bieber aliachia My World 2.0 wakati Snoop aliachia Malice N Wonderland.
Snoop amesema haofi kumface Bieber katika chart na mauzo sokono kwakuwa kazi zao zimetoka wakati mmoja ilia anachojali ni ushindani ambao anasema anaukaribisha kwani licha ya kuwa justin ni mkali lakini pia anaamini uwez wake katika kazi alizozitoa
Na amesema anaamini kazi zake zitafanya vizuri kama zinavyotakiwa kufanya

Wednesday, March 24, 2010

MDAU HEWANI...

Presenter wa TUMAINI TV (Arnord Nyambelwa mwiite Arnie Gizzle )Lakini piiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiia ni mdau mkubwa wa twentyfoursevenmishemishe.blogspot.com kama vipi zaidi mcheki jamaa kwenye himaya yake http://www.arniegizzle.blogspot.com/ .ONE.

FAMILIA YAKINA BEYONCE YAONGEZEKA...

Familia ya waimbaji Solange na Beyonce ikiwa chini ya mzee Mathew Knowles hivi sasa wameongezeka baada ya baba yao kupata mtoto mwingine wa kiume baada ya kufanyika vipimo vya DNA na kugundulika kuwa Nixon ambaye ni mtoto wa kiume aliyezaliwa na mama Alexsandra Wright aliyedai kuwa na mahusiano ya mzee Knowles kwa zaidi ya miezi 18 ni mtoto halisi wa baba yake beyonce
Oktoba mwaka jana mwanamama Wright alifungua kesi mahakamani na mzee akatakiwa kutoa dola 8,200 kila mwezi kwa ajili ya kumhudumia mtoto huyo hadi pale mambo yatakapowekwa hadhharani baada ya vipimo vya DNA kufanyika
Kutokana na tukio hilo January mwaka 2009 mama mzazi wa Beyoncé Tina Knowles alifungua kesi mahakamani akitaka talaka kutoka kwa mumewe huyo waliyeishi pamoja kwa zaidi ya miaka 30 na kufanikiwa kupata watoto wawili Beyonce aliye na miaka 28 na solange aliye na miaka 23

Tuesday, March 23, 2010

NICOLE NDANI YA "DANCING WITH THE STARS"

Nicole Scherzinger anafuata nyayo za wakali wengine wa kike Toni Braxton, Lil’ Kim, na Mya kwa kuwa msanii nyota wa muziki wa pop kujiunga katika kipindi cha “Dancing with the Stars.” Ambalo huonyeshwa nchini Marekani kwa nyota kadhaa kushindana kucheza wakiwa na partners zao na watazamaji huchagua mshindi kwa kutoa maksi
Hivi sasa piaa bongo kuna kipidi kama hicho ambacho hurushwa na TBC kinaitwa SEREBUKA na kuna mastaa kibao wanaoshiriki akiwemo mkali wa bongo flava kutoka temeke CHEGE na mwanabongo flava mwingine hemed na mwigizaji wa filamu irine uwoya

Monday, March 22, 2010

DRAKE"JAY Z NI MBADALA WA LIL WYNE.

Rapa Drake amesema jay z ni mtu anammaliza mawazo akimsikiliza kwenye ngoma zake muda huu ambao Lil Wayne yupo jela kutokana na mashairi yake yanayolenga kum-advice mtu .
Ikumbukwe kuwa lil wyne ndiye aliyemuibua drake kwa kumsainisha kwenye label ya young money mwaka jana mwishoni
Drake amesema amemkubali jayz baada ya kushirikiana naye katika album ya blueprint 3 na anatarajia kufanya naye kazi katika wimbo wa thank me later
“jay z anamsaidia sana kutokana na ushauri na maneno yake na ana vitu ambavyo ni tofauti na artist wengine” alisema drake

Friday, March 19, 2010

P DIDDY ANATAKA KUWA KAMA ABROMAVIC...

Sean “Diddy” Combs hivi sasa ana nia ya kuwekeza katika michezo hususani soka kwa kutaka kuinunuaclub ya soka ya Crystal Palace.Kwa mujibu wa Diddy anataka kujaribu kupata fursa hiyo ya kuinunua timu hiyo iliyo kusini mwa jiji la London kwa dau la paundi milioni 360 baada ya timu hiyo kufilisika mwaka huu mwezi january
Wakilithibitisha hilo wawakilishi wa rapper huyo wamesema ameangalia timu mbalimbali ili aweze kuzinunua lakini amevutiwa na Crystal Palace kutokana na jina lake hivyo ataungana na msanii mkongwe katika miondoko ya Hiphop Jayz ambaye anaendelea kujaribu kusaka soko la timu huko Ulaya
Ikumbukwe kuwa mwaka 2005 Jay-Z aliangalia uwezekano wa kuinunua Arsenal au timu ya Chelsea .Na endapo wazo la Diddy litafanikiwa basi atakuwa mkongwe wa kwanza wa hiphop kutoka Marekani kuwa mmiliki wa timu huko Ulaya

Thursday, March 18, 2010

CHAMILLIONAIRE"RAP SIO UHUNI.

Rapa kutoka kusini mwa nchi ya Marekani Chamillionaire ameelezea uwepo wa polisi wa hip-hop na kwa nini wasanii wanaorap wana tabia ya kuonyesha tabia za makosa ya jinai kupitia muziki. Chamillionaire amesema hivi sasa watu wengi wanashuhudia jinsi ambavyo wasanii wa rap wengi wanavyokwenda jela amesema ni tabia zao na si lifestyle ya muziki huu endapo mtu atakuwa akizungumzia masuala ya bunduki kila siku lazima maisha yake yatakuwa hivyo.
Naye produza wa kundi la Mobb Deep Alchemist naye pia amelizungumzia hilo na kusema marapa wanatofautiana na wengi huponzwa na marafiki mitaani, marafiki zao husababisha wajiingize katika biashara ya madawa ya kulevya wengine wakisikia VERSE zanazohusuyo bunduki hujua muziki wa rap unataka fujo jambo ambalo wanajidanganya na kusababisha hata polisi kujua kuwa marapa ni wahalifu

Wednesday, March 17, 2010

BEYONCE"MIMI NA J-Z NI ZAIDI YA SANA SIO KIDOGO.

Beyonce & Jay z
Beyoncé Knowles ametoa mambo muhimu kati yake na mumewe Jayz kwa kuwahamasisha wanawake kuolewa kwa ndoa ili kuweka mkataba maishani na si mkataba ndoa zinazodumu kwa muda mfupi za mkataba, beyonce amesema yeye na mumewe Jigga hawajaoana kwa majaribio anahitaji kuwa na watoto japo si sasa lakini baadaye na kuishi maisha ya nyumbani


Beyonce amesema maisha ya ndoa yakiwa kama ya wanafunzi wanaowategemea marafiki zao wa kiume kuwasaidia katika masuala mbalimbali hayana future yatakuwa na uoga ndani yake na mambo kama hayo yamewapoteza wanamuziki wengi muhimu ni kwa wasanii wanawake kufanya kazi kwa bidii na kuacha kuwategemea wanaume ili waweze kuwa na mapenzi ya kweli katika ndoa zao.

SWIZZ BEAT & ALICIA KEYS"MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA.

Kwa muda mrefu wawili hawa Alicia Keys and Swizz Beatz uhusuiano wao waliuweka siri lakini hivi sasa wakali hao kwenye game wameamua kuuonesha ulimwengu kuwa wanamahusiano.
kwa mara ya kwanza super-producer boyfriend Swizz Beatz alionekana hadharani akionesha upendo dhidi ya Alicia keys wakiti akipiga picha na gazeti la Gotham magazine’s huko New York City on Monday (March 15). Kwa pamoja wawili ho walionekana kuwa na furaha ambapo walipiga picha pamoja na mama mzazi wa Alicia Terri Augello na Busta Rhymes.

Tuesday, March 16, 2010

JUSTIN BIEBER NYOTA YAZIDI KUNG"ARA.

Wasichana wengi wanaguswa na msanii Bieber, wasichana wengi waigizaji ni mashabiki wakubwa wa mkali Bieber na mara nyingi wamekuwa wakimwalika katika show zao zaidi ya mara moja
Kwa mara ya kwanza katika historia ya program ya ABC katika kipindi cha miaka 13 msanii huyo ataonekana mara mbili katika kipindi jumatatu ijayo na jumanne akitarajiwa kuungana na Barbara Walters, Whoopi Goldberg, Elisabeth Hasselbeck na Sherri Shepherd kwa mahojiano maalum na kufanya tamasha
Mkali huyo kutoka Canada atakamua kazi yake ya “Never Let You Go” na kazi yake iliyoshika namba moja kati ya nyimbo 20 katika chati ya Baby .
Bado hazijafika hatawiki sita tangu mkali Justin Bieber aingie Islam Def jam na kuja na album yake ya My World na baada ya hapo akaimba kwa ajili ya Rais . Obama katika tamasha maalum la “We Are the World,” na kuwagusa wakali Rihana naBeyoncĂ©.

JIM JONES KUWATEACHER "NEW YORK CITY HIGH SKUL"

Diplomats rapper Jim Jones ameweka wazi kuwa kuanzia sasa ni wa limu New York City high school akifundisha muziki amesema kwake sio kazi ngumu sasa japo anatakiwa kusoma sasa kabla hajaingia kazini
The Dipset member amekubali kufundisha kwa muda wa wiki nne lakini hivi sasa bado hajanaanza kufundisha anachokifanya anareport kazini na kujifunnza baadhi ya vitu ambavyo atatakiwa kuanza kuvifanya na anasema anachosubili ni green light yani taa atakayomruhusu aanze kazi
Jones hajawi kupata kozi yeyote ya musiki kabla hivyo anahisi hiyo ni opffer kubwa kwake JONES alianza muziki tajgu akiwa mdogo na amepata mafanikio."katika muziki hivyo anamini kazi hiyo haiwezi kumshinda

Friday, March 12, 2010

WEEK-END NJEMA.

Bony sly ,glory & the man im self
hii ni baada ya kazi crew ya EBONY FM 2kibadilishana mawazo.

AKON KUFANYA TRACK YA KIHINDI.

Nyota wa muziki wa R&B Akon anafuata nyayo za mwanamuziki Snoop Dogg kwa kurekodi track itakayotumika katika filamu huko Bollywood
Rapa Snoop alirekodi wimbo kwa ajili ya filamu ya kihindi ya Singh is Kinng ulikuwa mwaka 2008 lakini Akon anakuja na kazi katika filamu yenye jina la RA na ataimba kwa lugha ya kihindi na amefanya kazi hiyo bure
Nyota wa Bollywood Shah Rukh Khan ambaye ameonekana katika filamu hiyo amesema Akon ataonekana katika filamu hiyo licha ya kuimba na sasa amesafiri kuelekea Mumbai India akiwa na familia yake, marafiki zake na timu ya wanamuziki
Akon amesema India ni nchi ambayo amekuwa na ndoto ya kufanya kazi na anahitaji kufanya vitu tofauti na kufurahia kazi yake ambayo ataifanya kiasili na kwa kutumia lugha asiyoizoea".

Tuesday, March 9, 2010

WYNE AANZA MAISHA YA JELA.

rapa Lil' Wayne ameanza maisha mapya ya mwaka mmoja jela baada ya kucheleweshwa kwa muda mrefu kupelekwa huko kutokana na kukutwa na silaha kinyume cha utaratibu kesi aliyoshtakiwa mwaka 2007
Mkali huyo wa The Lollipopr alipatikana na hatia mwaka jana ya kutaka kufanya uahalifu akiwa na silaha aliyokuwa nayo ikiwa na risasi 40 katika ziara kimuziki tena ndani ya basi
Mwezi uliopita alitarajiwa kuhukumiwa lakini hukumu hiyo ilihairishwa ili akafanyiwe upasuaji hivyo hukumu hiyo ilipangwa kukafanywa machi 2 na leo ndio hivyo tena kipenzi cha wengi amekwenda jela
Tathmini yaonyesha kuwa wakali wengi wa miondoko ya Hiphop hupitia maisha ya jela, kama 2PAC, DMX, ICE CUBE, DR DRE, SNOOP, COOLIO, BUSTER RYHMES, T.i na wengine wengi akiwemo Lil Wayne

Monday, March 8, 2010

KAA TAYARI KWA "RevelveR"YA T-MAUMIVU.

Mwimbaji ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya grammy T-Pain amewaambia mafanc wake kuwa album yake ya nne ijayo ya RevolveR itakuwa ya tofauti mbaya kwani hato wapa featuring wasanii wengi katika album hiyo


Album hiyo inatarajiwa kutoka mwezi ujao na itakuwa tofauti na album zilizopita kwa kuifanya solo zaidi ili mashabiki wapate utamu zaid amesema kuwa atafanya collabo na mwanamuziki wa miondoko ya country Carrie Underwood kwa kuwa ni muhimu

KEYSHIA COLE KUPATA MTOTO WA KIUME.....

Msanii Keyshia Cole amebahatika kupata mtoto wa kwanza wa kiume aliyezaa na mchumba wake mchezaji nyota wa basketball Daniel Gibson anayeitwa Daniel Hiram Gibson Jr.


Keyshia Cole aliweka wazi tetesi kuwa ana ujauzito wa star huyo wa kikapu wa Cleveland Cavaliers mwezi January mwaka huu na kuahidi kuwa wanatarajia kufunga ndoa baada ya kuvishana pete ya uchumba katika mkesha wa mwaka mpya na mchumba wake huyo.

Taarifa ya kujifungua Keyshia Cole inakuja baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini siku chache zilizopita baada ya kudhaniwa kuwa siku zake za kujifungua zimefika lakini mambo yalikuwa bado labda ulikuwa uoga flani kwa mtoto wa kwanza.